Tuesday, September 9, 2008

Face of Africa 2008


“Thank you, have a good day.”
Andiswa Manxiwa and Kaone Kario have been up since about 7AM, which is pretty late by the standards of the modelling world. If this past Saturday’s assignment had been a date with the flashy cameras of the beauty industry the ladies would have been up at 5AM so they could be at the location, made up and dressed up before the sun came up. Today the two girls in black are the judges whom the pretty young things, anxiously waiting outside the doors of the GICC have to impress if they are going to be entrants in this year’s Mnet Face of Africa model competition.

Of all the girls that showed up to the auditions, very few had an inkling of the kind of work that goes into a single modeling assignment.
The lack of that knowledge did not dampen the mood one single bit. On display was pure ambition. Dreams were on out on display for the unforgiving eye of the cameras, there to record the event for those with DStv. A rather disappointing 270 odd girls turned up for the audition which wasn’t fully representative of the sort of hotties you average connoisseur would like to see representing what they consider local beauty.

Most local guys probably feel these girls would give Kaone a serious run for her money. But what does the man on the street know about selecting models for an Africa wide model competition? It is a task best left to the professionals, and Kaone, albeit with a little well placed concern for the feelings of the hopefuls at first, was well up to the task.
Before all the girls could even go in to the judging room to be vetted on the basic requirements such as height, one or two girls got the elbow. The sharpness of the rejection must have been a little unreal with a video camera’s unblinking eye recording every nuance of the moment.

For us observers, it was awkwardly impressive to see the girls, Kaone and Andiswa, get to work immediately, demonstrating just how unforgiving modelling actually is. A nervous giggle twittered through the girls nearest to one of the unlucky girls. The first casualty looked very short next to Kaone, even when Kaone removed her stylish wooden platform sandals to stand bare foot.
The formalities dispatched with, it was time for the business of the day.

The remaining girls seeking fame and fortune registered and entered the interview room in groups of ten. The routine was simple, effective and model industry realistic. Height came first. A simple black line on the wall showed who measured up, if it were ever in doubt. Next up was a short catwalk strut in front of the two sharp eyed judges. The aspiring girls had to make that impression first time, if not, well, “Thank you. Have a good day.” And really that was it, no explanations, no discussions, and definitely no appeals.
Eleven girls made it through to the second round which involved swimsuits and left nothing in doubt as to body shapes and posture. From this final crop, Botswana’s representative will emerge.

The remaining girls were finally released after 6PM, leaving Kaone and Andiswa to continue with their long day agonising over who would be waving our flag high at the finals in Sun City. As for our strict and fantastically stylish judges, tomorrow it’s off to eleven more cities up and down the continent.

The mission: to gather the cream of the continent’s beauties for a fantastic modelling competition offering a grand opportunity, hopefully to girls named Tito or Gorata, who look set to be favourites in this humble reporter’s biased opinion.


Face of Africa 2008 – the fine print Model Scouts - Andiswa Manxiwa and Kaone Kario Countries to be Scouted - Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Mozambique, Namibia, Nigeria, South Africa, Tanzania, Uganda, and Zambia Boot camp in Zanzibar to be attended by a team featuring Oluchi as part of judges Finals night hosted at Suncity – 29 November 2008 The finals will be broadcast live on DStv Prizes include - 3 year modelling contract with former Face of Africa winner Oluchi USD 50.000 (US Dollars)
Olüchi Onweagba official website – www.oluchi.com

Model Africa website – www.omodelafrica.com

Mnet website – www.mnetafrica.com

Ay na P-square ndani ya studio za Hammy B

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Ambwene Yessaya ‘AY’ ameshakamilisha wimbo wake aliokuwa anataka kufanya na kundi la P-Square ambao hakutaka kuutaja, anashuka nayo Catherine Kassally.

Akichonga na Showbiz jijini Dar es Salaam, msanii huyo amesema kuwa wimbo huo umeshakamilika na ameufanya ndani ya studio za Hammy B za jijini Dar esa Salaam. AY amesema kuwa wimbo huo umeshakamilika na sasa yuko katika maandalizi ya kufanya video yake na kuongeza kuwa hivi karibuni anatarajia kwenda Lagos, Nigeria ambako ni makazi ya wasanii hao wanaounda kundi la P-Square linaloundwa na ndugu wawili ambao ni Paul na Peter.

Amesema kuwa wimbo huo hataki kuutaja jina kwa sasa kutokana na baadhi ya wasanii kuwa na tabia ya kudai nyimbo zilizotungwa na wenzao ni zao au mawazo yao.
“Unajua dunia imeharibika hasa kwa baadhi ya wasanii wanapoona mwenzao ametoa wimbo basi wanasema ni wao ndiyo maana sitautaja jina kwa sasa mpaka nitakapomalizia video yake na kuuachia katika vituo mbalimbali vya radio na televisheni ndiyo nitautaja jina lake,” alisema.

AY amesema mbali na kufanya wimbo huo yuko katika maandalizi ya albamu yake mpya ambayo ndani ya yake amewashirikisha wasanii mbalimbali wa hapa nyumbani na Kenya, Uganda na Afrika Kusini na amewataja kuwa ni pamoja na Chameleone, Nameless na Redson.

Foxy brown atinga jukwaani akiwa mjamzito

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Foxy Brown kwa sasa ni mjamzito. Habari kutoka mitandao mbalimbali nchini humo, zinasema kuwa mwanamuziki huyo ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki mwenzake wa Hip Hop, Rick Ross inawezekana akawa mhusika wa ujauzito huo.
Hivi karibuni, Foxy alitinga katika tamasha la utoaji tuzo za MTV katika jiji la New York akiwa na ujauzito wake. Msanii huyo ambaye kipindi cha nyuma alitamba na nyimbo zake kali, alikaa kimya na kuwafanya mashabiki wake ambao hawakumuona kwa muda mrefu katika onesho lolote kuhisi aliishiwa kisanii lakini aliwashangaza pale alipopanda jukwaani katika tuzo hizo na kufanya vitu vyake .

Fabulous ajiachia mitaani na mwanae

Ebwana hii itakuwa kali zaidi kwani hivi karibuni msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Fabolous hivi karibuni amebambwa na mapaparazi akiwa na mzazi mwenzake ambaye ni raia wa kilatin kimya kimya. Tukio lilitokea hivi karibuni huko New York nchini Marekani, ambapo mwanamuziki huyo akiwa na mwanadada huyo aliyezaa nae bila yeye kujijua.


Fabolous ameonekana kufurahishwa kuzaa na mlatino huyo ambapo kila mara msanii huyo amekuwa karibu na mwanae kitu ambacho kwake anakiona ni furaha kubwa. Lakini wadaku wanasema kuwa msanii huyo alikuwa hapendi watu wajui kama ana mtoto kutokana na kumficha ili mapaparazi wasijue.

Hata hivyo imeshindikana kumficha mtotot huyo kutokana na mashabiki wake kujua kinachoendelea na mwanadada huyo ila watu wanajiuliza msanii huyo aliyekuwa hapendi watu wajue ana mahusiano na mtu yeyote kwani alikuwa ni mzee wa totoz.

Wednesday, August 13, 2008

AFYA YA JAMII

UAMBUKIZO TUMBONI (ARO ENERITIS)


Uambukizo tumboni ni tatizo linalotokea katika tumbo la chakua. (Acute information of the lining of the stomach and intestine) uambukizo huu husambaa kuanzia katika tumbo la chakula hadi katika utumbo mwembamba na mkubwa.

Uambukizo huu huwa mkali (Acue gastroenteritis) inaweza kusababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi (Excusive indulgence in alcohol), uambukizo wa (virus, bacteria ingredients of food and dinks), mzio unaweza kusababishwa na vyakula na vinywaji. Pia zipo baadhi ya dawa zinazoweza kusababisha mzio pia yapo magonjwa mbalimbali yanayosababisha tatizo hili la uambukizo tumboni kama vile ugonjwa wa maumbo (typhoid fever), ugonjwa wa kuharisha damu, kipindupindu, kuungua mwili mzima na moto (Extensive burn).



DALILI ZA TATIZO


Dalili za tatizo hili huanza ghafla, mgonjwa huwa mchovu, hukoa hamu ya kula, hupatwa na kichefuchefu mara kwa mara, hutapika, tumbo huuma sana (Abdominal amps) ambapo misuli ya tumbo hukaza, uharisha, na mwili hulegea, uhisi moto au joto katika tundu ya haja kubwa (Retail burning and tenesmus), wakati mwingine hutokwa na majimaji yenye utelezi na damu katika njia ya haja kubwa. Mgonjwa hupata homa mgojwa akitapika na kuharisha sana hupoteza maji mwilini na kusababisa apoteze fahamu. Mgojwa huumwa kichwa, misuli hukaza na kuhisi ganzi mwili mzima.Tumbo huvimba na kujaa na akibonyezwa uhisi maumivu makali hasa chini ya kitovu.


UCHUNGUZI

Uchunguzi utategemea historia ya ugonjwa kama kuna kitu ulikula mfano pombe, maziwa, samaki, nyama au chakula chochote ambacho kilikutibua tumbo. Vipimo mbalimbali kama vipimo vya damu, haja kubwa na vipimo vingine ambavyo daktari ataona vinafaa. Mgonjwa atachunguzwa tumboni kuona athari zilizopo kwa kufanyiwa vipimo kama Ultrasound na sigmoidoscopy. Ugonjwa huu huathiri kuta za utumbo na hufanana na maradhi mengine kama ulcerative colitis na Amoebic dysentery.Ugonjwa huu pia hufanana na ugonjwa wa kidole tumbo na saratani ya utumbo (colonic malignancy)


MATIBABU

Mgonjwa apumzishwe, atapimwa vipimo mbalimbali kama vya damu, haja kubwa, shinikizo la damu, na mgonjwa ataongezewa maji. Atapatiwa tiba kufuatana na jinsi tatizo linavyojitokeza. Mgojwa atapewa dawa za kutuliza maumivu, kuzuia kuharisha na kutapika.


USHAURI

Ni vema uwahi hospitali kubwa kwa uchunguzi na tiba, kama tulivyoona, uchunguzi ni muhimu ili kujua chanzo cha tatizo na kukabiliana nacho. Epuka vyanzo vya tatizo zingatia tiba na kula chakula bora. Kunywa maji safi na salama. Kula chakua bora.

SAUZ KUMEKUCHA



Wadau hayo ndio maisha ya sauzi jee, unasemaje kuhusiana na hizo picha wewe una maoni gani?

Tuesday, August 12, 2008

KUMBUKUMBU YA COMPLEX AGOSTI 22, 2008

Wasanii kibao wa muziki wa kizazi kipya wanatarajia kumkumbuka Marehemu Simon Sayi "Complex" kupiti tamasha kubwa lenye jina la Remember litakalofanyika Agosti 22, mwaka huu ndani ya ukumbi wa Africentre, Ilala, Dar es Salaam, Christopher Lisa anashuka nayo.

Ndani ya safu hii mratibu wa tamasha hilo, George Alphonce "MC George" alisema kwamba, msanii Joan Matovolwa "Joan" ni miongoni mwa mastaa watakaokuwepo ndani ya tamasha hilo na tayari amesharekodi wimbo maalum kwa ajili ya siku hiyo.


"Joan" ambaye pia ni muigizaji wa luninga hivi sasa yupo katika mishemishe za kuitambulisha kazi hiyo ambayo ndani yake imewataja marehemu Complex na Stevie 2K, kupitia vituo mbalimbali vya redio. Wimbo huo umefanyika kupitia studio za Backyard, chini ya mtayarishaji Braton.

"Mbali na Joan, wasanii kama A.Y, Prof. Jay, Fid Q, Mwana FA, Wanaume Family, Wagosi wa Kaya, Dany Msimamo na wengine kibao wakiwemo wale waliowahi kufanya kazi na marehemu Complex watakuwepo siku hiyo, ambapo kwa heshima watapata nafasi ya kuongea mawili matatu kuhusu Complex", alisema George.


Aidha, mratibu huyo alisema kwamba, lengo la "Remember" ni kumkumbuka na kuyaenzi yale yote yaliyoachwa na marehemu kwa kuyaendeleza, kitu ambacho pia kitasaidia hata kizazi kijacho kuutambua mchango wake. Complex na aliyekuwa rafiki yake, Vivian Tilya walifariki katika ajali ya gari Agosti 21, 2005.

"Mbali na Complex, siku hiyo pia tutawakumbuka wasanii wote waliowahi kutoa mchango wao katika sanaa ya muziki nchini ambao tayari wametangulia mbele ya haki, itakuwa ni siku ya kipekee zaidi," alisema mratibu huyo.